Wednesday, 22 October 2014

Tembo hawatakidhi vizazi vijavyo

Tanzania ni miongoni mwa Nchi zilizobahatika kuwa na hifadhi zenye wanyama wazuri na wanaopendwa sana duniani. miongoni mwa wanyama hao ni Tembo na Twiga ambao wanapatikana karibu ndani ya hifadhi zote za hapa nchini.

Miaka ya hivi karibuni kumeibuka majangili ambao wanafanya biashara haramu ya kuua Wanyama hao na kuwasafirisha nje ya nchi , wakati mwingine kuwaua na kuchukua sehemu za miili yao kama pembe na meno yao ambayo yameonekana kuwa na thamani kubwa sana.

Pamoja na hayo wanaharakati pamoja viongozi wa Nchi wameonesha uzalendo kwa kupiga vita mauaji hayo ambayo kwa ujumla yanachafua sifa ya Tanzania na hata wakati mwingine kunapelekea watalii kukata tamaa ya kufika nchini kwani  ule uzuri wa mbuga wa kuvutia umekua unapotea kwa wanyama Tembo na Twiga ambao ndio wanawindwa kutoonekana kwa wingi.

Tembo ni wanyama wenye Thamani sana kwani meno yake mawili ni kama lulu kwa majangili ambao kila kukicha wanazidi kuwawinda na bila huruma kutumia silaha kama bunduki kwa ajili ya kuwawinda hali inayopelekea kuishi kwa wasi wasi mkubwa wawapo hifadhini

Swali linakuja kuwa je? ni kina nani wanahsika na Ujangili huu hatari sana, Mbuga zote zina walinzi ambao wameaminiwa na Serikali  kwa ajili ya kulinda Nyara hizo Je majangili hao wanapenyaje na kuondoka na Wanyama hao bila majangili kujulikana nawalinzi  kutodhurika? haya yanawezekana ni maswali ambayo kila mwananchi anajiuliza na majibu yake bado ni kitendawili kwa Taifa  zima.

Ni jukumu la kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzake na hata wakati mwingine kutoa taarifa iwapo unahisi kuna tendo au mtu mwenye matendo ya kijangili ili kuweza kuwanusuru wanyama hawa wachache waliobaki hapa nchini kwa ajili ya vizazi vijavyo.

 Takwimu mbalimbali zinathibitisha kwamba ndani ya mwaka mmoja zaidi ya Tembo  500 wanauawa hali inayopelekea hifadhi kubwa kama ya Ruaha na Serengeti kubaki na tembo wachache sana kuliko hapo awali hali inayotishia miaka  ijayo wanyama hao wanaweza kupotea kabisa katika hifadhi hapa nchini.   Bofya hapa kwa ufafanuzi zaidi http://archive.habarileo.co.tz/index.php/makala/20883-tanzania-bila-tembo-haiwezekani

Friday, 3 October 2014

warembo na utalii

miss utalii

Mashindano ya kumsaka miss utalii 2014/2015 yanarudi tena baada ya kusimama kwa mwaka mmoja kutokana na mipango ya awali kuwa na udhaifu katika kufanya maamuzi na kutafuta warembo wenye vigezo vya kuiwakilisha vyema Tanzania
Mashindano ya Urembo Tanzania ni mashindano yenye kubeba vigezo mbali mbali vya warembo hapa nchini. Ndani ya mashindano hayo yamegawanyika katika makundi tofauti tofauti na  yote yakiwa yana lengo kubwa moja la kumtoa mrembo awakalishe Nchi vyema kimataifa
 Miss utalii ni shindano linalomhusu mrembo wa kuuwakilisha utalii wa ndani ya nchini kimataifa kama jina la shindano lilivyo.Mara nyingi shindano hilo litahusisha warembo kutembelea hifadhi mbalimbali zilizopo ndani ya nchi
Mashindano haya hayafiki mbali kutokana na kwamba warembo hawapatiwi mafunzo ya kutosha juu ya shindano linahusu nini hivyo kushindwa kuiwakilisha nchi kama jinsi inavyotakiwa kufanyika kimataifa na pia kutokupewa mafunzo na hata baada ya shindano kumalizika.
warembo waliofanikiwa kuingia tano bora Miss utalii 2012/2013 katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Tanga Bi.Halima Bendego

Hata hivyo warembo wa mashindano haya bado hawajapewa nafasi au thamani kama inayowapasa kutokana na kuwakilisha Nchi kwa utambulisho wa utalii wa ndani na badala yake kubaki kuendelea kutaabika pamoja na kuwa na taji kubwa la kama mrembo wa Utalii Tanzania
Khadija Saidi akivalishwa taji la Miss Utalii Tanzania 2012/2013 na Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Tanga Bi.Halima Bendego kabla ya mashindano hayo kufungwa kwa mwaka mmoja


 Miss utalii tatu bora 2012/2013.katikati ni mshindi wa kwanza Khadija Said kulia ni Lucy Noel mshindi wa pili na kushoto ni Thelecia Kilomoa mshindi wa tatu 

Friday, 19 September 2014

Uzuri wa Katavi

Katavi ni moja ya hifadhi ya Taifa iliyopo Wilayani Mpanda, Mkoani Katavi. Hifadhi hii inasadikiwa kuwa ya tatu kwa ukubwa wake kati ya hifadhi zilizopo hapa  Nchini Tanzania

Pamoja na Mbuga ya Katavi kubeba Wanyama wengi ndani yake bado kuna vyanzo mbalimbali ambapo vinazidi kupendezesha Mbuga hiyo, ambapo Mito midogo midogo ndani yake nayo inatiririsha maji yake katika Ziwa Rukwa
Hifadhi ya Mbuga ya Katavi ikionekana na wanyama wapatikanao pamoja na Mito iliyopo ndani yake.
Watalii wengi wanafika Nchini kuangalia uzuri wa Hifadhi ya Katavi. Je? Watanzania wangapi wana desturi ya kutembelea hifadi zilizopo Nchini. Wanyama kama Twiga ni kati ya Wanyama wanaopatikana ndani ya Katavi na kwa uzuri wa Twiga ni kweli Katavi inastahili kupendeza na kuitwa Mbuga yenye kuvutia

Twiga Mnyama mwenye kuvutia ndani ya Hifadhi ya Katavi.
Tembo wapatikanao ndani ya hiadhi ya Katavi  wakinywa maji katika Mto upatikanao ndani ya Katavi.